UHURU WA MSHAIRI KATIKA USHAIRI WA KIARUDHI
Huu ni ule uwezo/ruhusa ya mshairi kutozingatia sheria za lugha ya nathari/mfululizo. Uhuru huu husaidia katika kuleta 1.usawa wa kimizani 2.mtiririko wa vina au muwala wa vina #Uhuru huu hujitokeza kupitia i) kuboronga sarufu. Hali ya kutozingatia taratibu za sarufi k.v kupangua mpagilia wa sentensi wa KN na KT. ii) utohozi Kuswahilisha maneno kutoka lugha zingine kama vile kiingereza -soksi,blanketing n.k iii) Tabdila Kubadilisha silabi ya mwisho ili kustawazisha urari wa vina bila kuathiri mizani. iv) Inkisari Kupunguza idadi ya silabi ili kustawazisha mizani. Mfano Nimemuona aliyenipenda - memuona alonipenda. v) Mazida/Mazda . Kurefusha/kuongeza silabi katika neno ili kusawazisha mizani. vi) kikale. Matumizi ya msamiati wa zamani ambao umesahaulika Maninga badala ya macho.